HABARI MPYA

IMANI YA CCM

  • Binadamu wote ni Sawa
  • Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
  • Ujamaa na kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru


AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI


(1) Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja


(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote


(3) Nitajitolera nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.


(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.


(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.


(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.


(7) Nitashjirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.


(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.


(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa CCM na raia mwema wa Tanzania na Afrika.