HABARI MPYA

Monday, November 5, 2012

MODENA ITALY:SHINA JIPYA LA CCM

CCM YASONGA MBELE ITALY!

Mwenyekiti wa shina Bi Mary Julius Mtemahanji katika picha ya pamoja na viongozi wa Tawi la CCM la Napoli Italy mara baada ya kuchaguliwa na wanachama wa CCM Modena katika ufunguzi wa shina la kwanza Italy.



 Bi Salama Kasiba akiangalia skafu ya CCM akiwa na katibu uchumi na Fedha wa tawi la CCM Napoli, ndugu FATUMA A.TANDIKA.
Pichani ni Mzee PASKAL NYALUS JONAS  (mjumbe) akiwa na Bi ESTHER EVAREST NGINGU (mjumbe)



Katibu wa Tawi la CCM la Napoli ndugu KAGUTTA NSANGU MAULIDI akitoa hotuba kufafanua katiba ya chama juu ya utaratibu wa shina na taratibu za uchaguzi. Pamoja nae katikati ni Mwenyekiti wa Tawi la CCM la Napoli Ndugu ABDULRAHAMAN A. ALLI na Katibu wa uchumi na fedha ndugu FATUMA A.TANDIKA

Tarehe 3/11/2012 itabaki katika  historia ya Chama cha Mapinduzi ughaibuni , baada ya kufunguliwa shina la kwanza nchini Italy. Ufunguzi huo ulisimamiwa na kuendeshwa na viongozi wa Tawi la Napoli ambalo ni tawi pekee nchini Italy.Wanachama wa CCM Modena  walimchagua Bi MARY  JULIUS MTEMAHANJI kuwa Mwenyekiti, baada ya mchuano mkali wa kura kati yake na ndugu PASKAL NYALUSI JONAS ambaye baadae alichaguliwa kuwa mjumbe wa kamati ya uongozi. Wengine waliochaguliwa ni Katibu wa shina ndugu MWINYIMWAKA HATIBU SARAI, bi HALIMA MWEVI, Bi SALAMA KASIBA, na Bi LEYLA  RAYMOND walichaguli kama wajumbe wa kamati ya uongozi.

No comments:

Post a Comment